1. Je! Mtu hana wakati wake wa vita juu ya nchi?Na siku zake, je! Si kama siku za mwajiriwa?
2. Kama mtumishi atamaniye sana kile kivuli,Kama mwajiriwa anayetazamia mshahara wake;
3. Ni vivyo nami nimepewa miezi ya ubatili iwe fungu langu,Nami nimeandikiwa masiku yenye kuchokesha.
4. Hapo nilalapo chini, nasema,Nitaondoka lini? Lakini usiku huwa mrefu;Nami nimejawa na kujitupa huku na huku hata kupambazuke.