9. Kwamba Mungu angekuwa radhi kuniseta;Kwamba angeulegeza mkono wake na kunikatilia mbali!
10. Hapo ndipo ningefarijika hata sasa;Naam, ningejikuza katika maumivu yasiyoniacha;Kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11. Nguvu zangu ni zipi, hata ningoje?Na mwisho wangu ni nini, hata nisubiri?
12. Je! Nguvu zangu ni nguvu za mawe?Au mwili wangu, je! Ni shaba?
13. Je! Si kwamba sina msaada ndani yangu.Tena kwamba kufanikiwa kumeondolewa mbali nami?
14. Kwake huyo atakaye kuzima roho inapasa atendewe mema na rafiki;Hata kwake huyo aachaye kumcha Mwenyezi.
15. Ndugu zangu wametenda udanganyifu kama kijito cha maji.Mfano wa fumbi la vijito vipitavyo.
16. Vilivyokuwa vyeusi kwa sababu ya barafu,Ambamo theluji hujificha.
17. Wakati vipatapo moto hutoweka;Kukiwako hari, hukoma mahali pao.
18. Misafara isafiriyo kwa njia yao hugeuka;Hukwea kwenda barani, na kupotea.
19. Misafara ya Tema huvitazama,Majeshi ya Sheba huvingojea.
20. Wametahayari kwa sababu walitumaini;Wakaja huku, nao walifadhaika.
21. Kwani sasa ninyi mmekuwa vivyo;Mwaona jambo la kutisha, mkaogopa.
22. Je! Nilisema, Nipeni?Au, Nitoleeni toleo katika mali yenu?
23. Au, Niokoeni na mkono wa adui?Au, Nikomboeni na mikono ya hao waoneao?
24. Nifunzeni, nami nitanyamaa kimya;Mkanijulishe ni jambo gani nililokosa.