6. Je! Kitu kisicho na ladha yumkini kulika pasipo chumvi?Au je, uto wa yai una tamu iwayo yote?
7. Roho yangu inakataa hata kuvigusa;Kwangu mimi ni kama chakula kichukizacho.
8. Laiti ningepewa haja yangu,Naye Mungu angenipa neno hilo ninalolitamani sana!
9. Kwamba Mungu angekuwa radhi kuniseta;Kwamba angeulegeza mkono wake na kunikatilia mbali!
10. Hapo ndipo ningefarijika hata sasa;Naam, ningejikuza katika maumivu yasiyoniacha;Kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.