Ayu. 6:6-10 Swahili Union Version (SUV)

6. Je! Kitu kisicho na ladha yumkini kulika pasipo chumvi?Au je, uto wa yai una tamu iwayo yote?

7. Roho yangu inakataa hata kuvigusa;Kwangu mimi ni kama chakula kichukizacho.

8. Laiti ningepewa haja yangu,Naye Mungu angenipa neno hilo ninalolitamani sana!

9. Kwamba Mungu angekuwa radhi kuniseta;Kwamba angeulegeza mkono wake na kunikatilia mbali!

10. Hapo ndipo ningefarijika hata sasa;Naam, ningejikuza katika maumivu yasiyoniacha;Kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.

Ayu. 6