5. Je! Huyo punda-mwitu hulia akiwa na majani?Au, ng’ombe hulia malishoni?
6. Je! Kitu kisicho na ladha yumkini kulika pasipo chumvi?Au je, uto wa yai una tamu iwayo yote?
7. Roho yangu inakataa hata kuvigusa;Kwangu mimi ni kama chakula kichukizacho.
8. Laiti ningepewa haja yangu,Naye Mungu angenipa neno hilo ninalolitamani sana!
9. Kwamba Mungu angekuwa radhi kuniseta;Kwamba angeulegeza mkono wake na kunikatilia mbali!
10. Hapo ndipo ningefarijika hata sasa;Naam, ningejikuza katika maumivu yasiyoniacha;Kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11. Nguvu zangu ni zipi, hata ningoje?Na mwisho wangu ni nini, hata nisubiri?
12. Je! Nguvu zangu ni nguvu za mawe?Au mwili wangu, je! Ni shaba?