Ayu. 6:27-30 Swahili Union Version (SUV)

27. Naam, mwapenda kuwapigia kura hao mayatima,Na kufanya biashara ya rafiki yenu.

28. Sasa basi iweni radhi kuniangalia;Kwani hakika sitanena uongo usoni penu.

29. Rudini, nawasihi, lisiwe neno la udhalimu;Naam, rudini tena, neno langu ni la haki.

30. Je! Mna udhalimu ulimini mwangu?Je! Makaakaa yangu hayatambui mambo ya madhara?

Ayu. 6