27. Naam, mwapenda kuwapigia kura hao mayatima,Na kufanya biashara ya rafiki yenu.
28. Sasa basi iweni radhi kuniangalia;Kwani hakika sitanena uongo usoni penu.
29. Rudini, nawasihi, lisiwe neno la udhalimu;Naam, rudini tena, neno langu ni la haki.
30. Je! Mna udhalimu ulimini mwangu?Je! Makaakaa yangu hayatambui mambo ya madhara?