Ayu. 6:26-30 Swahili Union Version (SUV)

26. Je! Mwafikiri kuyakemea maneno?Maana maneno ya huyo aliyekata tamaa ni kama upepo.

27. Naam, mwapenda kuwapigia kura hao mayatima,Na kufanya biashara ya rafiki yenu.

28. Sasa basi iweni radhi kuniangalia;Kwani hakika sitanena uongo usoni penu.

29. Rudini, nawasihi, lisiwe neno la udhalimu;Naam, rudini tena, neno langu ni la haki.

30. Je! Mna udhalimu ulimini mwangu?Je! Makaakaa yangu hayatambui mambo ya madhara?

Ayu. 6