Ayu. 6:21-26 Swahili Union Version (SUV)

21. Kwani sasa ninyi mmekuwa vivyo;Mwaona jambo la kutisha, mkaogopa.

22. Je! Nilisema, Nipeni?Au, Nitoleeni toleo katika mali yenu?

23. Au, Niokoeni na mkono wa adui?Au, Nikomboeni na mikono ya hao waoneao?

24. Nifunzeni, nami nitanyamaa kimya;Mkanijulishe ni jambo gani nililokosa.

25. Jinsi yafaavyo maneno ya uelekevu!Lakini kuhoji kwenu, je! Kumeonya nini?

26. Je! Mwafikiri kuyakemea maneno?Maana maneno ya huyo aliyekata tamaa ni kama upepo.

Ayu. 6