Ayu. 5:9-14 Swahili Union Version (SUV)

9. Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana;Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;

10. Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi,Na kuyapeleka maji mashambani;

11. Awainuaye juu hao walio chini;Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.

12. Yeye huyatangua mashauri ya wadanganyifu,Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao.

13. Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao wenyewe;Na mashauri ya washupavu yaharibika kwa haraka.

14. Wao hupatwa na giza wakati wa mchana,Hupapasa mchana vilevile kama usiku.

Ayu. 5