Ayu. 5:6-13 Swahili Union Version (SUV)

6. Kwani taabu haitoki mchangani,Wala mashaka hayachipuki katika nchi;

7. Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate mashaka,Kama cheche za moto zirukavyo juu.

8. Lakini mimi ningemtafuta Mungu,Ningemwekea Mungu daawa yangu;

9. Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana;Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;

10. Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi,Na kuyapeleka maji mashambani;

11. Awainuaye juu hao walio chini;Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.

12. Yeye huyatangua mashauri ya wadanganyifu,Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao.

13. Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao wenyewe;Na mashauri ya washupavu yaharibika kwa haraka.

Ayu. 5