13. Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao wenyewe;Na mashauri ya washupavu yaharibika kwa haraka.
14. Wao hupatwa na giza wakati wa mchana,Hupapasa mchana vilevile kama usiku.
15. Lakini yeye huokoa na upanga wa kinywa chao,Hata kumwokoa mhitaji na mkono wake aliye hodari.
16. Basi hivi huyo maskini ana matumaini,Na uovu hufumba kinywa chake.