1. Haya, ita sasa; je! Yuko atakayekujibu?Nawe utamwelekea yupi katika hao watakatifu?
2. Kwani hasira humwua mtu mpumbavu,Nao wivu humwua mjinga.
3. Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi;Lakini mara niliyalaani maskani yake.
4. Watoto wake wako mbali na wokovu,Nao wamesongwa langoni,Wala hapana atakayewaponya.
5. Mavuno yake wale wenye njaa huyala,Na kuyatwaa hata kuyatoa miibani,Nao wenye kiu huzitwetea mali zao.