1. Haya, ita sasa; je! Yuko atakayekujibu?Nawe utamwelekea yupi katika hao watakatifu?
2. Kwani hasira humwua mtu mpumbavu,Nao wivu humwua mjinga.
3. Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi;Lakini mara niliyalaani maskani yake.
4. Watoto wake wako mbali na wokovu,Nao wamesongwa langoni,Wala hapana atakayewaponya.