Ayu. 5:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Haya, ita sasa; je! Yuko atakayekujibu?Nawe utamwelekea yupi katika hao watakatifu?

2. Kwani hasira humwua mtu mpumbavu,Nao wivu humwua mjinga.

3. Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi;Lakini mara niliyalaani maskani yake.

4. Watoto wake wako mbali na wokovu,Nao wamesongwa langoni,Wala hapana atakayewaponya.

Ayu. 5