Ayu. 42:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Ndipo Ayubu akamjibu BWANA, na kusema.

2. Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote,Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.

3. Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa?Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu,Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua.

4. Sikiliza, nakusihi, nami nitanena;Nitakuuliza neno, nawe niambie.

5. Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio;Bali sasa jicho langu linakuona.

Ayu. 42