1. Ndipo Ayubu akamjibu BWANA, na kusema.
2. Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote,Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.
3. Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa?Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu,Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua.