26. Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii;Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.
27. Yeye huona chuma kuwa kama nyasi,Na shaba kama mti uliooza.
28. Mshale hauwezi kumkimbiza;Na mawe ya teo kwake hugeuka kuwa kama makapi.
29. Marungu huhesabiwa kama mabua;Naye hucheka mshindo wa mkuki ukitupwa.
30. Pande zake za chini ni kama vigae vikali;Hutandika malazi kama kuweka chombo cha kupuria nafaka juu ya matope.
31. Yeye huchemsha kilindi mfano wa nyungu;Hufanya bahari kuwa kama mafuta.
32. Hufanya mapito yake kung’aa nyuma yakeHata mtu angedhani kilindi kina mvi.
33. Juu ya nchi hapana aliyefanana naye,Aliyeumbwa pasipo oga.