21. Pumzi zake huwasha makaa,Na miali ya moto hutoka kinywani mwake.
22. Katika shingo yake hukaa nguvu,Na utisho hucheza mbele yake.
23. Manofu ya nyama yake hushikamana;Yanakazana juu yake; hayawezi kuondolewa.
24. Moyo wake una imara kama jiwe;Naam, imara kama jiwe la chini la kusagia.
25. Anapojiinua, mashujaa huogopa;Kwa sababu ya woga wao huvunjwa moyo.
26. Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii;Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.
27. Yeye huona chuma kuwa kama nyasi,Na shaba kama mti uliooza.
28. Mshale hauwezi kumkimbiza;Na mawe ya teo kwake hugeuka kuwa kama makapi.
29. Marungu huhesabiwa kama mabua;Naye hucheka mshindo wa mkuki ukitupwa.
30. Pande zake za chini ni kama vigae vikali;Hutandika malazi kama kuweka chombo cha kupuria nafaka juu ya matope.
31. Yeye huchemsha kilindi mfano wa nyungu;Hufanya bahari kuwa kama mafuta.
32. Hufanya mapito yake kung’aa nyuma yakeHata mtu angedhani kilindi kina mvi.