Ayu. 41:17-23 Swahili Union Version (SUV)

17. Yamefungamana pamoja;Yameshikamana, hata hayawezekani kutengwa.

18. Kwa kuchemua kwake mwanga humemetuka,Na macho yake yanafanana na makope ya alfajiri.

19. Mienge iwakayo hutoka kinywani mwake,Na macheche ya moto huruka nje.

20. Moshi hutoka katika mianzi ya pua yake,Kama nyungu ikitokota, na manyasi yawakayo.

21. Pumzi zake huwasha makaa,Na miali ya moto hutoka kinywani mwake.

22. Katika shingo yake hukaa nguvu,Na utisho hucheza mbele yake.

23. Manofu ya nyama yake hushikamana;Yanakazana juu yake; hayawezi kuondolewa.

Ayu. 41