Ayu. 40:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Ndipo Ayubu akamjibu Mungu, na kusema,

4. Tazama, mimi si kitu kabisa, nikujibu nini?Naweka mkono wangu kinywani pangu.

5. Nimenena mara moja, nami sitajibu;Naam, nimenena mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.

6. Ndipo BWANA akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,

7. Jifunge viuno kama mwanamume,Mimi nitakuuliza neno, nawe niambie.

Ayu. 40