3. Ndipo Ayubu akamjibu Mungu, na kusema,
4. Tazama, mimi si kitu kabisa, nikujibu nini?Naweka mkono wangu kinywani pangu.
5. Nimenena mara moja, nami sitajibu;Naam, nimenena mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.
6. Ndipo BWANA akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,
7. Jifunge viuno kama mwanamume,Mimi nitakuuliza neno, nawe niambie.