21. Hulala chini ya miti yenye vivuli,Mafichoni penye mianzi, na matopeni.
22. Hiyo miti yenye vivuli humfunika kwa vivuli vyao;Mierebi ya vijito humzunguka.
23. Tazama, mto ukifurika, yeye hatetemeki;Hujiona yu salama, ijapokuwa Yordani hufurika hata kinywani pake.
24. Je! Mtu ye yote atamnasa akiwa yu macho,Au, kumtoboa pua yake kwa mtego?