Ayu. 40:21-24 Swahili Union Version (SUV)

21. Hulala chini ya miti yenye vivuli,Mafichoni penye mianzi, na matopeni.

22. Hiyo miti yenye vivuli humfunika kwa vivuli vyao;Mierebi ya vijito humzunguka.

23. Tazama, mto ukifurika, yeye hatetemeki;Hujiona yu salama, ijapokuwa Yordani hufurika hata kinywani pake.

24. Je! Mtu ye yote atamnasa akiwa yu macho,Au, kumtoboa pua yake kwa mtego?

Ayu. 40