18. Tazama, yeye hawategemei watumishi wake;Na malaika zake huwahesabia upuzi;
19. Je! Si zaidi sana hao wakaao katika nyumba za udongo,Ambazo misingi yao i katika mchanga,Hao waliosetwa mbele ya nondo!
20. Kati ya asubuhi na jioni huvunjwa-vunjwa;Waangamia milele wala hapana atiaye moyoni.
21. Je! Kamba ya hema yao haikung’olewa ndani yao?Wafa, kisha hali hawana akili.