14. Hofu iliniangukia na kutetema,Iliyoitetemesha mifupa yangu yote.
15. Ndipo pepo ilipita mbele ya uso wangu;Na nywele za mwili wangu zilisimama.
16. Hiyo pepo ilisimama kimya, nisiweze kutambua sura zake,Mfano ulikuwa mbele ya macho yangu;Kulikuwa kimya, nami nilisikia sauti, ikinena,
17. Je! Binadamu atakuwa na haki kuliko Mungu?Je! Mtu atakuwa safi kuliko Muumba wake?
18. Tazama, yeye hawategemei watumishi wake;Na malaika zake huwahesabia upuzi;