Ayu. 39:6-11 Swahili Union Version (SUV)

6. Ambaye nimeifanya nyika kuwa nyumba yake,Na nchi ya chumvi kuwa makao yake.

7. Yeye hudharau mshindo wa mji,Wala hasikii kelele zake msimamizi.

8. Upana wa milima ni malisho yake,Hutafuta-tafuta kila kitu kilicho kibichi.

9. Je! Nyati atakubali kukutumikia?Au atakaa katika zizi lako?

10. Je! Waweza kumfunga nyati kwa kamba matutani?Au, yeye atayalima mabonde nyuma yako?

11. Je! Utamtumaini kwa sababu ana nguvu nyingi?Au, utamwachia yeye kazi yako?

Ayu. 39