26. Je! Mwewe huruka juu kwa akili zako,Na kuyanyosha mabawa yake kwenda kusini?
27. Je! Tai hupaa juu kwa amri yako,Na kufanya kioto chake mahali pa juu?
28. Hukaa jabalini, ndiko kwenye malazi yake,Juu ya genge la jabali, na ngomeni.
29. Toka huko yeye huchungulia mawindo;Macho yake huyaangalia toka mbali.
30. Makinda yake nayo hufyonza damu;Na kwenye maiti ndiko aliko.