2. Je! Waweza kuhesabu miezi yao watakayoitimiza?Au je! Wajua majira ya kuzaa kwao?
3. Wao hujiinamisha, kuzaa watoto wao,Watupa taabu zao.
4. Watoto wao wa katika hali nzuri, hukua katika bara wazi;Huenda zao, wala hawarudi tena.
5. Ni nani aliyempeleka punda-milia aende huru?Au je! Ni nani aliyemfungulia vifungo punda-mwitu?
6. Ambaye nimeifanya nyika kuwa nyumba yake,Na nchi ya chumvi kuwa makao yake.
7. Yeye hudharau mshindo wa mji,Wala hasikii kelele zake msimamizi.
8. Upana wa milima ni malisho yake,Hutafuta-tafuta kila kitu kilicho kibichi.