Ayu. 39:13-20 Swahili Union Version (SUV)

13. Bawa la mbuni hufurahi;Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma?

14. Kwani yeye huyaacha mayai yake juu ya nchi,Na kuyatia moto mchangani,

15. Na kusahau kwamba yumkini mguu kuyavunja,Au mnyama wa mwitu kuyakanyaga.

16. yeye huyafanyia ukali makinda yake, kana kwamba si yake;Ijapokuwa taabu yake ni ya bure, hana hofu;

17. Kwa sababu Mungu amemnyima akili,Wala hakumpa fahamu.

18. Wakati anapojiinua juu aende,Humdharau farasi na mwenye kumpanda.

19. Je! Wewe ulimpa farasi uwezo wake?Au, ni wewe uliyemvika shingo yake manyoya yatetemayo?

20. Ndiwe uliyemfanya aruke kama nzige?Fahari ya mlio wake hutisha.

Ayu. 39