Ayu. 37:8-15 Swahili Union Version (SUV)

8. Hapo wanyama huingia mafichoni,Na kukaa katika mapango yao.

9. Dhoruba hutoka katika vyumba vyake;Na baridi ghalani mwake.

10. Barafu huletwa kwa pumzi za Mungu;Na upana wa maji huganda.

11. Naam, huyatweka mawingu mazito mzigo wa maji;Hulitandika wingu la umeme wake;

12. Nalo hugeuzwa huku na huku kwa uongozi wake,Ili yafanye yote atakayoyaagizaJuu ya uso wa dunia hii ikaayo watu;

13. Kama ni kwa kuonya, au kama ni kwa nchi yake,Au kama ni kwa rehema, ndiye aletaye.

14. Sikiliza neno hili, Ee Ayubu;Simama kimya, uzifikiri kazi za Mungu za ajabu.

15. Je! Wajua wewe jinsi Mungu anavyoziagiza,Na kuumulikisha umeme wa wingu lake?

Ayu. 37