Ayu. 37:4-14 Swahili Union Version (SUV)

4. Baadaye sauti hunguruma;Yeye hunguruma kwa sauti ya ukuu wake;Hazizuii hapo sauti yake isikiwapo.

5. Mungu hunguruma kwa kustaajabisha kwa sauti yake;Hufanya mambo makuu, ambayo hatuwezi kuelewa nayo.

6. Kwani huiambia theluji, Anguka juu ya nchi;Na vivyo manyonyota ya mvua,Na hayo maji ya mvua yake kubwa.

7. Huufunga mkono wa kila binadamu;Ili watu wote aliowaumba wajue.

8. Hapo wanyama huingia mafichoni,Na kukaa katika mapango yao.

9. Dhoruba hutoka katika vyumba vyake;Na baridi ghalani mwake.

10. Barafu huletwa kwa pumzi za Mungu;Na upana wa maji huganda.

11. Naam, huyatweka mawingu mazito mzigo wa maji;Hulitandika wingu la umeme wake;

12. Nalo hugeuzwa huku na huku kwa uongozi wake,Ili yafanye yote atakayoyaagizaJuu ya uso wa dunia hii ikaayo watu;

13. Kama ni kwa kuonya, au kama ni kwa nchi yake,Au kama ni kwa rehema, ndiye aletaye.

14. Sikiliza neno hili, Ee Ayubu;Simama kimya, uzifikiri kazi za Mungu za ajabu.

Ayu. 37