3. Yeye huituma iende chini ya mbingu zote,Na radi yake hata miisho ya nchi.
4. Baadaye sauti hunguruma;Yeye hunguruma kwa sauti ya ukuu wake;Hazizuii hapo sauti yake isikiwapo.
5. Mungu hunguruma kwa kustaajabisha kwa sauti yake;Hufanya mambo makuu, ambayo hatuwezi kuelewa nayo.
6. Kwani huiambia theluji, Anguka juu ya nchi;Na vivyo manyonyota ya mvua,Na hayo maji ya mvua yake kubwa.
7. Huufunga mkono wa kila binadamu;Ili watu wote aliowaumba wajue.
8. Hapo wanyama huingia mafichoni,Na kukaa katika mapango yao.
9. Dhoruba hutoka katika vyumba vyake;Na baridi ghalani mwake.
10. Barafu huletwa kwa pumzi za Mungu;Na upana wa maji huganda.
11. Naam, huyatweka mawingu mazito mzigo wa maji;Hulitandika wingu la umeme wake;
12. Nalo hugeuzwa huku na huku kwa uongozi wake,Ili yafanye yote atakayoyaagizaJuu ya uso wa dunia hii ikaayo watu;