Ayu. 37:3-12 Swahili Union Version (SUV)

3. Yeye huituma iende chini ya mbingu zote,Na radi yake hata miisho ya nchi.

4. Baadaye sauti hunguruma;Yeye hunguruma kwa sauti ya ukuu wake;Hazizuii hapo sauti yake isikiwapo.

5. Mungu hunguruma kwa kustaajabisha kwa sauti yake;Hufanya mambo makuu, ambayo hatuwezi kuelewa nayo.

6. Kwani huiambia theluji, Anguka juu ya nchi;Na vivyo manyonyota ya mvua,Na hayo maji ya mvua yake kubwa.

7. Huufunga mkono wa kila binadamu;Ili watu wote aliowaumba wajue.

8. Hapo wanyama huingia mafichoni,Na kukaa katika mapango yao.

9. Dhoruba hutoka katika vyumba vyake;Na baridi ghalani mwake.

10. Barafu huletwa kwa pumzi za Mungu;Na upana wa maji huganda.

11. Naam, huyatweka mawingu mazito mzigo wa maji;Hulitandika wingu la umeme wake;

12. Nalo hugeuzwa huku na huku kwa uongozi wake,Ili yafanye yote atakayoyaagizaJuu ya uso wa dunia hii ikaayo watu;

Ayu. 37