Ayu. 37:20-24 Swahili Union Version (SUV)

20. Je! Aambiwe kwamba nataka kunena?Au mtu angetamani kumezwa?

21. Na sasa watu hawawezi kuutazama mwanga ung’aao mbinguni;Lakini upepo ukipita huzitakasa.

22. Kaskazini hutokea umemetufu wa dhahabu;Mungu huvikwa ukuu utishao.

23. yeye Mwenyezi hamwezi kumwona;Yeye ni mkuu mwenye uweza;Tena mwenye hukumu, na mwingi wa haki, hataonea.

24. Kwa hiyo watu humwogopa;Yeye hawaangalii walio na hekima mioyoni.

Ayu. 37