2. Zisikizeni hizo kelele za sauti yake,Na uvumi utokao kinywani mwake.
3. Yeye huituma iende chini ya mbingu zote,Na radi yake hata miisho ya nchi.
4. Baadaye sauti hunguruma;Yeye hunguruma kwa sauti ya ukuu wake;Hazizuii hapo sauti yake isikiwapo.
5. Mungu hunguruma kwa kustaajabisha kwa sauti yake;Hufanya mambo makuu, ambayo hatuwezi kuelewa nayo.
6. Kwani huiambia theluji, Anguka juu ya nchi;Na vivyo manyonyota ya mvua,Na hayo maji ya mvua yake kubwa.
7. Huufunga mkono wa kila binadamu;Ili watu wote aliowaumba wajue.