10. Barafu huletwa kwa pumzi za Mungu;Na upana wa maji huganda.
11. Naam, huyatweka mawingu mazito mzigo wa maji;Hulitandika wingu la umeme wake;
12. Nalo hugeuzwa huku na huku kwa uongozi wake,Ili yafanye yote atakayoyaagizaJuu ya uso wa dunia hii ikaayo watu;
13. Kama ni kwa kuonya, au kama ni kwa nchi yake,Au kama ni kwa rehema, ndiye aletaye.