5. Tazama, Mungu ni hodari, wala hamdharau mtu ye yote;Ana uweza katika nguvu za fahamu.
6. Hauhifadhi uhai wa waovu;Lakini huwapa wateswao haki yao.
7. Yeye hawaondolei macho yake wenye haki;Lakini pamoja na wafalme huwawekaKatika viti vya enzi milele, nao hutukuzwa.
8. Nao wakifungwa kwa pingu,Wakitwaliwa kwa kamba za mateso;
9. Ndipo huwaonyesha matendo yao,Na makosa yao, ya kuwa wametenda kwa kujivuna.
10. Yeye huyafunua masikio yao, wasikie maonyo,Na kuwaagiza warudi kuuacha uovu.
11. Kama wakisikia na kumtumikia,Watapisha siku zao katika kufanikiwa,Na miaka yao katika furaha.
12. Lakini wasiposikia, wataangamia kwa upanga,Nao watakufa pasipo maarifa.
13. Lakini hao wasiomcha Mungu mioyoni hujiwekea hasiraHawalilii msaada hapo awafungapo.
14. Wao hufa wakali vijana,Na uhai wao huangamia katikati ya wachafu.
15. Yeye humponya aliyetaabika kwa njia ya taabu yake,Na kuyafunua masikio yao kwa maonevu.
16. Naam, yeye angekuongoza utoke katika msibaHata mahali penye nafasi, ambapo hapana msonge;Na kilichowekwa mezani pako kingejaa mafuta.
17. Lakini umejaa hukumu ya waovu;Hukumu na haki hukushika.