4. Kwani yakini maneno yangu si ya uongo;Aliyekamilika katika maarifa yu pamoja nawe.
5. Tazama, Mungu ni hodari, wala hamdharau mtu ye yote;Ana uweza katika nguvu za fahamu.
6. Hauhifadhi uhai wa waovu;Lakini huwapa wateswao haki yao.
7. Yeye hawaondolei macho yake wenye haki;Lakini pamoja na wafalme huwawekaKatika viti vya enzi milele, nao hutukuzwa.
8. Nao wakifungwa kwa pingu,Wakitwaliwa kwa kamba za mateso;
9. Ndipo huwaonyesha matendo yao,Na makosa yao, ya kuwa wametenda kwa kujivuna.