Ayu. 36:27-33 Swahili Union Version (SUV)

27. Kwani yeye huvuta juu matone ya maji,Yamwagikayo katika mvua kutoka kungeni mwake;

28. Ambayo mawingu yainyeshaNa kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi.

29. Naam, mtu aweza kuelewa na matandazo ya mawingu,Ngurumo za makao yake?

30. Tazama, yeye huutandaza mwanga wake, umzunguke;Naye hufunika vilindi vya bahari.

31. Kwani huwahukumu kabila za watu kwa njia hizi;Hutoa chakula kwa ukarimu.

32. Yeye huifunika mikono yake kwa umeme;Na kuuagiza shabaha utakayopiga.

33. Mshindo wake hutoa habari zake,Anayewaka hasira juu ya uovu.

Ayu. 36