26. Tazama, Mungu ni mkuu, nasi hatumjui;Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27. Kwani yeye huvuta juu matone ya maji,Yamwagikayo katika mvua kutoka kungeni mwake;
28. Ambayo mawingu yainyeshaNa kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi.
29. Naam, mtu aweza kuelewa na matandazo ya mawingu,Ngurumo za makao yake?
30. Tazama, yeye huutandaza mwanga wake, umzunguke;Naye hufunika vilindi vya bahari.
31. Kwani huwahukumu kabila za watu kwa njia hizi;Hutoa chakula kwa ukarimu.
32. Yeye huifunika mikono yake kwa umeme;Na kuuagiza shabaha utakayopiga.
33. Mshindo wake hutoa habari zake,Anayewaka hasira juu ya uovu.