Ayu. 36:19-28 Swahili Union Version (SUV)

19. Je! Mali yako yatatosha, hata usiwe katika taabu,Au uwezo wote wa nguvu zako?

20. Usiutamani usiku,Wakati watu wakatwapo katika mahali pao.

21. Jitunze, usiutazame uovu;Kwani umeuchagua huo zaidi ya taabu.

22. Tazama, Mungu hutenda makuu kwa uweza wake;Ni nani afundishaye kama yeye?

23. Ni nani aliyemwagiza njia yake?Au ni nani awezaye kusema, Wewe umetenda yasiyo haki?

24. Kumbuka kuitukuza kazi yake,Watu waliyoiimbia.

25. Wanadamu wote wameitazama;Watu huiangalia kwa mbali

26. Tazama, Mungu ni mkuu, nasi hatumjui;Hesabu ya miaka yake haitafutiki.

27. Kwani yeye huvuta juu matone ya maji,Yamwagikayo katika mvua kutoka kungeni mwake;

28. Ambayo mawingu yainyeshaNa kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi.

Ayu. 36