Ayu. 35:8-16 Swahili Union Version (SUV)

8. Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe;Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.

9. Kwa sababu ya wingi wa jeuri wao hulia;Walilia msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.

10. Wala hapana asemaye, Yuko wapi Mungu Muumba wangu,Awapaye nyimbo wakati wa usiku;

11. Atufundishaye zaidi ya hayawani wa nchi,Na kutufanya wenye hekima kuliko ndege za angani?

12. Hulia huko, lakini hapana ajibuye,Kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.

13. Hakika Mungu hatasikia ubatili,Wala Mwenyezi hatauangalia.

14. Sembuse usemapo wewe ya kuwa humwangalii,Hiyo daawa i mbele yake, nawe wamngojea!

15. Lakini sasa, kwa sababu yeye hakukujilia katika hasira zake,Wala hauangalii sana unyeti;

16. Ndiposa Ayubu hufunua kinywa chake kwa ubatili;Huongeza maneno pasipo maarifa.

Ayu. 35