Ayu. 35:5-12 Swahili Union Version (SUV)

5. Ziangalie mbingu ukaone;Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe.

6. Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake?Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?

7. Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani?Au yeye hupokea nini mkononi mwako?

8. Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe;Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.

9. Kwa sababu ya wingi wa jeuri wao hulia;Walilia msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.

10. Wala hapana asemaye, Yuko wapi Mungu Muumba wangu,Awapaye nyimbo wakati wa usiku;

11. Atufundishaye zaidi ya hayawani wa nchi,Na kutufanya wenye hekima kuliko ndege za angani?

12. Hulia huko, lakini hapana ajibuye,Kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.

Ayu. 35