1. Tena Elihu akajibu na kusema,
2. Je! Wewe wadhani kwamba haya ni haki yako,Au je! Wasema, Haki yangu ni zaidi kuliko ya Mungu,
3. Maana wasema, Kutakuwa na faida gani kwako wewe?Tena, Nitapata faida gani, kuliko nikifanya dhambi?
4. Mimi nitakujibu,Na hawa wenzio pamoja nawe.
5. Ziangalie mbingu ukaone;Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe.
6. Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake?Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?
7. Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani?Au yeye hupokea nini mkononi mwako?