Ayu. 34:30-36 Swahili Union Version (SUV)

30. Kwamba huyo mpotovu asitawale,Pasiwe na wa kuwatega watu.

31. Kwani kuna mtu aliyemwambia Mungu,Mimi nimevumilia kurudiwa, ingawa sikukosa;

32. Nisiyoyaona nifundishe wewe;Kama nimefanya uovu sitafanya tena?

33. Je! Malipo yake yatakuwa kama upendavyo wewe, hata ukayakataa?Kwani yakupasa wewe kuchagua, si mimi;Kwa sababu hiyo sema uyajuayo.

34. Watu walio na akili wataniambia,Naam, kila mtu mwenye hekima anisikiaye;

35. Huyo Ayubu amesema pasipo maarifa,Na maneno yake hayana hekima.

36. Laiti Ayubu angejaribiwa hata mwisho,Kwa kuwa amejibu kama watu waovu.

Ayu. 34