Ayu. 34:3-8 Swahili Union Version (SUV)

3. Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno,Kama vile kaakaa lionjavyo chakula.

4. Na tujichagulie yaliyo ya uelekevu;Na tujue wenyewe yaliyo mema.

5. Kwani Ayubu amesema, Mimi ni mwenye haki,Naye Mungu ameniondolea haki yangu;

6. Nijapokuwa mwenye haki, nimehesabiwa kuwa mwongo;Jeraha yangu haiponyeki, nijapokuwa sina makosa.

7. Je! Ni mtu gani mfano wa Ayubu,Anywaye mzaha kama maji?

8. Atembeaye na hao watendao uovu,Na kwenda pamoja na watu wabaya.

Ayu. 34