Ayu. 34:3-18 Swahili Union Version (SUV)

3. Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno,Kama vile kaakaa lionjavyo chakula.

4. Na tujichagulie yaliyo ya uelekevu;Na tujue wenyewe yaliyo mema.

5. Kwani Ayubu amesema, Mimi ni mwenye haki,Naye Mungu ameniondolea haki yangu;

6. Nijapokuwa mwenye haki, nimehesabiwa kuwa mwongo;Jeraha yangu haiponyeki, nijapokuwa sina makosa.

7. Je! Ni mtu gani mfano wa Ayubu,Anywaye mzaha kama maji?

8. Atembeaye na hao watendao uovu,Na kwenda pamoja na watu wabaya.

9. Kwa kuwa amenena, Haimfai mtu lo loteKujifurahisha na Mungu.

10. Kwa hiyo nisikilizeni, enyi wenye fahamu;Mungu asidhaniwe kutenda udhalimu;Wala Mwenyezi kufanya uovu.

11. Kwani atamlipa binadamu kwa kazi yake,Naye atamfanya kila mtu kuona sawasawa na njia zake

12. Naam, hakika, Mungu hatatenda mabaya,Wala Mwenyezi hatapotosha hukumu.

13. Ni nani aliyemwagiza kuiangalia dunia?Au ni nani aliyemwekea ulimwengu huu wote?

14. Kama akimwekea mtu moyo wake,Akijikusanyia roho yake na pumzi zake;

15. Wenye mwili wote wataangamia pamoja,Nao wanadamu watarejea tena kuwa mavumbi.

16. Ikiwa una ufahamu, sikia neno hili;Isikilize sauti ya maneno yangu.

17. Je! Atatawala mtu aichukiaye haki hata mmoja?Nawe, je! Utamhukumia mkosa aliye na haki na mwenye nguvu?

18. Je! Inafaa kumwambia mfalme, Wewe u mwovu?Au kuwaambia wakuu, Ninyi ni wabaya?

Ayu. 34