Ayu. 34:14-21 Swahili Union Version (SUV)

14. Kama akimwekea mtu moyo wake,Akijikusanyia roho yake na pumzi zake;

15. Wenye mwili wote wataangamia pamoja,Nao wanadamu watarejea tena kuwa mavumbi.

16. Ikiwa una ufahamu, sikia neno hili;Isikilize sauti ya maneno yangu.

17. Je! Atatawala mtu aichukiaye haki hata mmoja?Nawe, je! Utamhukumia mkosa aliye na haki na mwenye nguvu?

18. Je! Inafaa kumwambia mfalme, Wewe u mwovu?Au kuwaambia wakuu, Ninyi ni wabaya?

19. Sembuse huyo asiyependelea nyuso za wakuu,Wala hawajali matajiri kuliko maskini?Kwani wote ni kazi ya mikono yake,

20. Hufa ghafula, hata usiku wa manane;Watu hutikisika na kwenda zao,Nao mashujaa huondolewa pasipo mkono wa mtu.

21. Kwani macho yake ya juu ya njia za mtu,Naye huiona miendo yake yote.

Ayu. 34