11. Kwani atamlipa binadamu kwa kazi yake,Naye atamfanya kila mtu kuona sawasawa na njia zake
12. Naam, hakika, Mungu hatatenda mabaya,Wala Mwenyezi hatapotosha hukumu.
13. Ni nani aliyemwagiza kuiangalia dunia?Au ni nani aliyemwekea ulimwengu huu wote?
14. Kama akimwekea mtu moyo wake,Akijikusanyia roho yake na pumzi zake;
15. Wenye mwili wote wataangamia pamoja,Nao wanadamu watarejea tena kuwa mavumbi.
16. Ikiwa una ufahamu, sikia neno hili;Isikilize sauti ya maneno yangu.
17. Je! Atatawala mtu aichukiaye haki hata mmoja?Nawe, je! Utamhukumia mkosa aliye na haki na mwenye nguvu?
18. Je! Inafaa kumwambia mfalme, Wewe u mwovu?Au kuwaambia wakuu, Ninyi ni wabaya?
19. Sembuse huyo asiyependelea nyuso za wakuu,Wala hawajali matajiri kuliko maskini?Kwani wote ni kazi ya mikono yake,
20. Hufa ghafula, hata usiku wa manane;Watu hutikisika na kwenda zao,Nao mashujaa huondolewa pasipo mkono wa mtu.
21. Kwani macho yake ya juu ya njia za mtu,Naye huiona miendo yake yote.
22. Hapana weusi, wala hilo giza tupu,Wawezapo kujificha watendao udhalimu.