Ayu. 34:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Tena Elihu akajibu na kusema,

2. Sikilizeni maneno yangu, enyi wenye hekima;Tegeni masikio kwangu, ninyi mlio na maarifa.

3. Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno,Kama vile kaakaa lionjavyo chakula.

4. Na tujichagulie yaliyo ya uelekevu;Na tujue wenyewe yaliyo mema.

5. Kwani Ayubu amesema, Mimi ni mwenye haki,Naye Mungu ameniondolea haki yangu;

6. Nijapokuwa mwenye haki, nimehesabiwa kuwa mwongo;Jeraha yangu haiponyeki, nijapokuwa sina makosa.

7. Je! Ni mtu gani mfano wa Ayubu,Anywaye mzaha kama maji?

Ayu. 34