28. Yeye ameikomboa nafsi yangu isiende shimoni,Na uhai wangu utautazama mwanga.
29. Tazama, hayo yote ni Mungu anayeyafanya,Mara mbili, naam, hata mara tatu, kwa mtu,
30. Ili kurudisha roho yake itoke shimoni,Ili atiwe mwanga kwa mwanga wa walio hai.
31. Angalia sana, Ee Ayubu, unisikilize;Nyamaza, mimi nitasema.
32. Kama una neno la kusema, nijibu;Nena, kwani nataka kukuhesabia kuwa na haki.
33. Kama sivyo, unisikilize mimi;Nyamaza, nami nitakufunza hekima.