Ayu. 33:2-7 Swahili Union Version (SUV)

2. Tazama basi, nimefunua kinywa changu,Ulimi wangu umenena kinywani mwangu.

3. Maneno yangu yatatamka uelekevu wa moyo wangu;Na hayo niyajuayo midomo yangu itayanena kwa unyofu.

4. Roho ya Mungu imeniumba,Na pumzi za Mwenyezi hunipa uhai.

5. Kwamba waweza, nijibu;Yapange maneno yako sawasawa mbele yangu, usimame.

6. Tazama, mimi ni mbele ya Mungu kama ulivyo wewe;Mimi nami nilifinyangwa katika udongo.

7. Tazama, utisho wangu hautakutia hofu wewe,Wala sitakulemea kwa uzito.

Ayu. 33