15. Katika ndoto, katika maono ya usiku,Usingizi mzito uwajiliapo watu,Katika usingizi kitandani;
16. Ndipo huyafunua masikio ya watu,Na kuyatia muhuri mafundisho yao,
17. Ili amwondoe mtu katika makusudio yake,Na kumfichia mtu kiburi;
18. Yeye huizuia nafsi yake isiende shimoni,Na uhai wake usiangamie kwa upanga.
19. Yeye hutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake,Na kwa mashindano yaendeleayo daima mifupani mwake;
20. Hata roho yake huchukia chakula,Na nafsi yake huchukia nyama nzuri.
21. Nyama ya mwili wake huliwa, isionekane;Na mifupa yake isiyoonekana yatokea nje.
22. Naam, nafsi yake inakaribia shimoni,Na uhai wake unakaribia waangamizi.
23. Kwamba akiwapo malaika pamoja naye,Mkalimani, mmoja katika elfu,Ili kumwonyesha binadamu hayo yampasayo;
24. Ndipo amwoneapo rehema, na kusema,Mwokoe asishuke shimoni;Mimi nimeuona ukombozi.
25. Nyama ya mwili wake itakuwa laini kuliko ya mtoto;Huzirudia siku za ujana wake;