Ayu. 33:15-25 Swahili Union Version (SUV)

15. Katika ndoto, katika maono ya usiku,Usingizi mzito uwajiliapo watu,Katika usingizi kitandani;

16. Ndipo huyafunua masikio ya watu,Na kuyatia muhuri mafundisho yao,

17. Ili amwondoe mtu katika makusudio yake,Na kumfichia mtu kiburi;

18. Yeye huizuia nafsi yake isiende shimoni,Na uhai wake usiangamie kwa upanga.

19. Yeye hutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake,Na kwa mashindano yaendeleayo daima mifupani mwake;

20. Hata roho yake huchukia chakula,Na nafsi yake huchukia nyama nzuri.

21. Nyama ya mwili wake huliwa, isionekane;Na mifupa yake isiyoonekana yatokea nje.

22. Naam, nafsi yake inakaribia shimoni,Na uhai wake unakaribia waangamizi.

23. Kwamba akiwapo malaika pamoja naye,Mkalimani, mmoja katika elfu,Ili kumwonyesha binadamu hayo yampasayo;

24. Ndipo amwoneapo rehema, na kusema,Mwokoe asishuke shimoni;Mimi nimeuona ukombozi.

25. Nyama ya mwili wake itakuwa laini kuliko ya mtoto;Huzirudia siku za ujana wake;

Ayu. 33