Ayu. 32:7-12 Swahili Union Version (SUV)

7. Nilisema, Yafaa siku ziseme,Na wingi wa miaka ufundishe hekima.

8. Lakini imo roho ndani ya mwanadamu,Na pumzi za Mwenyezi huwapa akili.

9. Sio wakuu walio wenye akili,Wala sio wazee watambuao hukumu.

10. Basi nilisema, Nisikilizeni mimi;Mimi nami nitawaonyesha nionavyo.

11. Tazama, niliyangojea maneno yenu,Nilizisikiliza nisikie hoja zenu,Hapo mlipokitafuta mtakalonena.

12. Naam, niliwasikiza ninyi,Na tazama, hapana mmoja aliyemshinda Ayubu,Wala kumjibu maneno yake, kati yenu.

Ayu. 32