4. Basi huyo Elihu alikuwa anangoja ili anene na Ayubu, kwa sababu hao wengine walikuwa wazee kuliko yeye.
5. Hata Elihu alipoona kuwa hapana jawabu katika vinywa vya watu hao watatu, hasira zake ziliwaka.
6. Basi Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi, akajibu, na kusema,Mimi ni kijana, na ninyi ni wazee sana;Kwa hiyo nilijizuia, nisithubutu kuwaonyesha nionavyo.
7. Nilisema, Yafaa siku ziseme,Na wingi wa miaka ufundishe hekima.
8. Lakini imo roho ndani ya mwanadamu,Na pumzi za Mwenyezi huwapa akili.
9. Sio wakuu walio wenye akili,Wala sio wazee watambuao hukumu.
10. Basi nilisema, Nisikilizeni mimi;Mimi nami nitawaonyesha nionavyo.
11. Tazama, niliyangojea maneno yenu,Nilizisikiliza nisikie hoja zenu,Hapo mlipokitafuta mtakalonena.
12. Naam, niliwasikiza ninyi,Na tazama, hapana mmoja aliyemshinda Ayubu,Wala kumjibu maneno yake, kati yenu.
13. Jitunzeni msiseme, Sisi tumepata hekima;Mungu yumkini akamshinda, si mtu;
14. Kwa kuwa yeye hajayaelekeza maneno yake kwangu;Wala sitamjibu mimi kwa maneno yenu.
15. Wameshangaa, hawajibu tena;Hawana neno la kusema.
16. Na mimi, je! Ningoje, kwa sababu hawaneni,Kwa sababu wasimama kimya, wala wasijibu tena;